
MTOTO ALIYETOWEKA APATIKANA BUNGOMA
Familia moja kutoka kijiji cha Kamasielo kaunti ya Bungoma ilifurahia baada ya kuunganishwa na mtoto wao aliyeibiwa katika hospitali ya Kimilili baada ya kuzaliwa miezi mbili iliyopita. Bungoma: Mtoto aliyetoweka baada ya mamake kumzaa kupitia njia ya upasuaji apatikana
Mtoto huyo alipatikana na wauguzi waliokuwa wakiendesha zoezi la kupeana chanjo katika wadi ya Maeni siku ya Ijumaa, Oktoba 29. Afisa mkuu wa afya katika hospitali ya kata ndogo ya Kimilili David Shivachi alisema wauguzi walitilia shaka baada ya mshukiwa kukosa kuwasilisha cheti cha kuzaliwa na stakabathi muhimu za mtoto huyo
Baada ya kufanya vipimo vya DNA, ilibainika kwamba mtoto huyo alikuwa wa Ruth ambaye alitoweka Septemba 15 pindi baada ya mamake kumzaa kupitia njia ya upasuaji.
Baada ya kuondoka thieta niliuliza nilitewe mtoto nimuone alafu nikaambiwa kwamba ametoweka, nilishtuka sana kama mama, lakini sai nimefurahi na namshukuru Mungu kwa kumpata, kwa hivyo nitampa jina King David,” Mama huyo aliambia wanahabari. Nakhumisha alianza kuhisi uchungu wa uzazi Septemba 15, alipofika katika hospitali ya Kimilili, madaktari walimshauri ajifungue kupitia njia ya upasuaji kwa sababu alikuwa na matatizo ambayo hangeweza kujifungua kawaida.
ulikuja hapa asubuhi na mke wangu akapelekwa thieta mwendo wa saa tano asubuhi, nilisubiri nje madaktari wakihudumia mke wangu, madaktari walishinda wakiniambia niwe na subira kwa sababu nilikuwa nimeanza kushikwa na wasiwasi. Dakika chache baadaye mmoja wao aliniambie kwamba mtoto ameibiwa,” Mume wa Nakhumicha alielezea. Familia hiyo iliwashukuru wauguzi hao pamoja na hospitali ya Kimilili kwa kuwasaidia kumpata mtoto wao
