Meneja wa habari na mawasiliano wa Klabu ya Simba Ahmed Ally amesema Simba kwasasa inapitia kwenye kipindi kigumu ambacho timu nyingi kubwa huwa zinapitia hata hivyo amewaambia mashabiki na wanachama wa Simba kuwa hawatamaliza ligi kinyonge
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ahmed Ally ameandika
“..Imewalazimu AC Millan kusubiri miaka 11 wakiutafuta Ubingwa wa Italia (Serie A)
Wamebadilisha wachezaji wengi, na wamebadilisha makocha wengi hatimae Stefano Pioli amekuja kuwafuta machozi
Kocha Pioli aliyewapa ubingwa hakua chaguo la mashabiki wa AC Millan, walimkataa tangu siku ya kwanza ya uteuzi wake
Mabango yalitawala kila kona ya Sansiro yameendikwa Pioli Out lakini baada ya muda mabango yaleyale yakaandikwa Pioli you are hero
Kwenye mpira timu kubwa hupitia MSOTO, AC Millan wamepitia msoto wa miaka 11
Vivyo hivyo kwa timu yetu Simba msimu huu tunapitia MSOTO
Na mara nyingi msoto hua unapatikana baada ya mafanikio makubwa kwenye timu
Zipo sababu nyingi zinazopelekea timu kupitia wakati mgumu, kwanza kuchoka kwa wachezaji, kupotea kwa kiu ya mafanikio, kupungua ubora kwa wachezaji au majeruhi yaliyotokana na wachezaji kutumika kwa muda mrefu
Kitu muhimu ni kutambua mapema kwanini unapitia wakati mgumu, utafute suluhu ya haraka ili MSOTO usiwe mrefu kama wa AC Millan
Wana Simba wenzangu msifadhaishwe na mapito haya na wala msibabaishwe na kelele za malimbukeni
Wao wamepitia msoto mkali wa miaka mitano ambapo Simba hatuwezi kusota kwa kiwango hicho Insha Allah
Pamoja na yote lakini hatutamaliza msimu kinyonge”
Simba wamepata alama 2 kwenye michezo miwili iliyopita ya ligi kuu ya NBC na kuzima ndoto za kutetea taji hilo msimu huu.
