Mshambuliaji wa Brazil Neymar amefunga bao moja katika ushindi wa mabao 4-1 waliopata Brazil dhidi ya timu ya Uruguay katika michezo ya kufuzu kombe la dunia mwakani nchini Qatar. Goli hilo la Neymar inamfanya afikishe goli 70 kwenye timu ya taifa. Mfungaji bora wa muda wote wa timu ya taifa ya Brazil ni gwiji Pele aliyefunga magoli 77. Hivyo hadi Sasa Neymar amezidiwa goli Saba kufikia rekodi hiyo ya Pele.